Wednesday, December 5, 2012


 
Wakili  wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Vitalis Timon, ameiambia Mahakama ya Rufani kuwa waliopinga matokeo ya ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, hawakuwa na haki ya kufanya hivyo kisheria na kwamba matusi, kejeli na kashfa haviwezi kumvua nafasi hiyo.

Alidai kuwa matusi hayawezi kumvua ubunge Lema kwani wabunge wenyewe walitunga sheria namba nane ya mwaka 1995 ikiruhusu matusi baada ya kuona awali kuwa walikuwa wakibanwa na mahakama.

Wakili Timon alitoa madai hayo katika Mahakama ya Rufani mbele ya jopo la majaji watatu lililowajumuisha Jaji Nathalia Kimaro, Salum Massati na Benard Luanda, waliposikiliza rufaa iliyowasilishwa na Lema akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Arusha wa kumvua ubunge.

Lema alivuliwa ubunge Aprili 5 mwaka huu kufuatia kesi iliyofunguliwa na wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel.

“Wapiga kura hawawezi kupinga matokeo ya uchaguzi wakati yanayotokea katika kampeni hayawahusu, mpiga kura si sehemu ya kamati ya maadili na hana haki katika kampeni...katika ushahidi walalamikaji walidai kwamba walimshauri Batilda (aliyekuwa mgombea wa CCM) kwa muda mrefu afike mahakamani, alikataa ndipo wakaamua kwenda wao mahakamani,” alidai na kuongeza kuwa:

“Julai 31, 1995 Bunge lilipitisha sheria namba nane wakisema kwamba matusi si sababu ya kutengua matokeo, wenyewe Wabunge waliruhusu watukanane katika sheria waliyotunga, wanapenda kutukanana, wabunge walijipendelea wakati wakitunga sheria hiyo baada ya kuona mahakama inawabana katika eneo hilo, waacheni watukanane waliyataka wenyewe,” alidai wakili huyo mwandamizi wa serikali.

Timon alidai kuwa wanaohusika wakati wa kampeni ni wagombea, vyama vya siasa, mawakala wa wagombea na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na kwamba wapiga kura wanahusika kulalamikia hatua za usajili wa wapiga kura na wakati wa kupiga kura.

 “Waheshimiwa majaji, waliokuwa na maslahi binafsi katika kesi hii ni waliopoteza jimbo. Baada ya uchaguzi CCM walikaa kikao na kuazimia kulirudisha jimbo kwa kufungua kesi, walikuwa na nia mbaya walipofungua shauri hili,” aliendelea kuieleza mahakama.

“Sioni kwa nini Jaji wa Arusha aseme Lema alikuwa na maslahi binafsi katika ushahidi wake kwa kuleta wanachama wa Chadema kutoa ushahidi, angewaleta watu gani zaidi ya hao waliokuwapo wakati wa kampeni?” alihoji.

 “CCM walileta mashahidi wa CCM, lakini hawakuambiwa kwamba walikuwa na maslahi binafsi, naunga mkono rufaa na naomba uamuzi wa kumvua Lema ubunge utenguliwe,” aliiambia mahakama.

Wakili wa Lema, Method Kimomogolo, akizungumzia hoja 18 za kukata rufaa hiyo, alidai kwamba Jaji aliyetoa hukumu ya kumvua ubunge Lema, Gabriel Rwakibarila, alikosea kisheria kuvutiwa na njia walizotumia shahidi wa 11 na 14 badala ya kuzingatia uzito wa ushahidi waliotoa.

 “Alivutiwa na shahidi wa 11 Amina Ally ambaye anaishi kwa kuuza mitumba na shahidi wa 14 ambaye alitumikia jeshi nje ya nchi na akastaafu kwa kuogopa kupelekwa tena nje ya nchi,” alidai Kimomogolo.

“Jaji alikosea kuegemea katika ushahidi usioaminika na ushahidi wa mdomo bila kutafuta ushahidi mwingine wa kuunga mkono hivyo kuifanya hukumu kutokidhi vigezo vya kuitwa hukumu,” alidai Kimomogolo.

Kimomogolo alidai kuwa Jaji Rwakibarila wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga katika hukumu yake hakutumia mifano ya kesi mbalimbali zilizoamuliwa na Mahakama ya Rufaa, japo alipelekewa ili azirejee na mawakili wa pande zote mbili.

Kimomogolo aliendelea kulieleza jopo hilo la majaji kuwa Jaji Rwakibarila hakuchanganua wala kupima ushahidi licha ya kuwasilishiwa viini vikuu vilivyokuwa vinabishaniwa.

“Mrufani hakuwahi kukamatwa na Polisi wakati wa kampeni kwa kutukana na jaji hakusema makosa gani ya jinai yalitendwa na mrufani katika kampeni zake,” alidai.

Alidai kuwa uamuzi uliomvua ubunge Lema ukikubaliwa na kuruhusu kila mtu apinge matokeo ya uchaguzi kwa kufungua kesi, hali itakuwa mbaya na kuongeza kuwa mtu afike mahakamani kwa malalamiko yanayomhusu.

“Jukumu la kutetea maslahi ya Taifa ni la Mwanasheria Mkuu wa Serikali, si wanachama wa CCM waliopinga ubunge, kama wanaona AG hafanyi kazi vizuri, wananchi wamwajibishe,” alidai.

Wakili Kimomogolo alirejea kesi mbalimbali zinazofanana na kesi ya Lema ikiwamo ya Joseph Warioba dhidi ya Stephen Wassira, Basil Mramba dhidi ya Leonce Ngalai, William Bakari dhidi ya Mgonja na kesi ya Walid Kabourou  iliyoamuliwa miaka 16 iliyopita na watu waliwasilisha hadi `tape' mahakamani.

“Kwa nini katika kesi ya Lema wajibu rufani hawakuwasilisha hata ushahidi wa `tape' kuonyesha matusi aliyotukana?” alihoji Kimomogolo.

Wakili wa wajibu rufani, Alute Mughway, alidai mashahidi wao walieleza kila kitu mahakamani na jaji alikuwa anajua nani mwenye jukumu la kuthibitisha kesi.

Alidai kuwa ushahidi uliotolewa haukupaswa kuungwa mkono na ushahidi wowote na kwamba siasa za uchaguzi zinatakiwa kuwa safi kwani hata katika kanuni za uchaguzi wanaonywa kuhusu matusi, kejeli na kudhalilishana.

“Siasa za matusi ni siasa za maji taka zilikatazwa, kanuni zilizokataza zilisainiwa na vyama vyote, watu wanachaguliwa kwa hoja si kungurumisha matusi na kuwadhalilisha wagombea wengine,” alidai Mughway.

Alidai kuwa hukumu ilikidhi viwango vyote na kuomba rufaa itupiliwe mbali kwa sababu zilizotolewa na mrufani hazitoshelezi kutengua uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

“Waheshiwa, tunaomba uamuzi wa Mahakama ya Arusha ubaki kama ulivyokuwa na warufani waamuriwe kulipa gharama za kesi,” alidai. Kesi iliahirishwa hadi tarehe ya hukumu itakapopangwa.

 Akizungumza katika viunga vya mahakama hiyo baada ya kuahirishwa kesi hiyo, Lema aliwasihi wanachama wake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu wakati wanasubiri hukumu.

“Hiki ni kipindi kigumu wakati tunasubiri hukumu kutolewa kuliko tulipokuwa tunasubiri usikilizwaji wa rufaa hii, nawasihi muwe na utulivu kwani kila mmoja amesikia mahakamani mawakili walivyotoa hoja zao,” alidai Lema.

Aliwataka kuwa watulivu waiachie mahakama ifanye kazi yake kwa mujibu wa sheria na kwamba haki itatendeka.

Mapema saa 2:00 asubuhi, viunga vya mahakama hiyo vilifurika wafuasi wa Chadema wakiongozwa na Lema waliofika kusikiliza kesi hiyo pamoja na wananchi mbalimbali.

Ukumbi namba moja wa mahakama hiyo ulifunguliwa saa 2:30 asubuhi na saa 3:00 asubuhi  jopo hilo liliketi chini na kuanza kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi jopo litakapopanga tarehe ya hukumu kama Lema atarudishiwa ubunge wake ama la.

Tuesday, December 4, 2012

WIKI, moja baada  ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra) kupokea maoni ya kuongezeka kwa nauli za mabasi yaendayo mikoani kutoka kwa wadau wa usafiri, nauli za mabasi hayo zinadaiwa kuanza kupanda.

Habri   kutoka kwa baadhi ya makarani wa kampuni za mabasi yaendayo  mikoani katika Kituo Kikuu cha Mabasi yaendeyo mikoani Ubungo (UBT), jijini Dar es Salaam zinaelza  kuwa nauli zimeanza kupanda hasa kwa magari yaendayo mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

“Baadhi ya magari yanayokwenda mikoani yameshaanza kuongeza nauli toka Shilingi20, 000 na 22,000 hadi 25,000 kwa magari yaendayo  Arusha na Kilimanjaro.”

Kwa mujibu wa makarani hao  sio mabasi yote  yenye tabia ya kupandisha nauli kiholela hasa katika kipindi cha kuelekea sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

Hidaya Hassan, karani Kampuni ya Basi ya Tashrif ambayo mabasi yake yanafanya safari kati ya Dar es Salaam na Tanga, alisema nauli zinaweza kupanda kuanzia mwezi huu kwa kuwa kipindi hiki kunakuwapo na idadi kubwa ya abiria wanaotaka kusafiri kwenda mikoani huku idadi ya magari ikiwa ni ndogo.

Shekha Lema, karani Kampuni ya Basi ya Master City Ltd ambayo mabasi yake  yanafanya safari kati ya Dar es Salaam na Mwanza na maeneo mengine, alisema nauli bado hazijaanza kupanda kwani inakuwa vigumu kwao kufanya hivyo kwa kuwa hata vitabu vyenyewe vya risiti vimegongwa muhuri na abiria ni wachache.

“Sisi mabasi ya kampuni yetu yanayofanya safari kati ya Dar na Mwanza, nauli bado ni ile ile ya Sh.35, 400, hatuwezi kuibadilisha,” alisema Lema na kuongeza:

Baadhi ya makarani hao pia, wamedai kuwa upandishwaji holela wa nauli haufanywi na kampuni bali hufanywa na madalali ambao hununua tiketi na kuwauzia abiria kwa bei kubwa na matokeo yake Sumatra inapokagua wanaolaumiwa ni kampuni, jambao ambalo wamesema si kweli.

“Upandishwaji wa nauli kiholela ni kama vile mfumuko wa bei za vitu au bidhaa masokoni. Madalali ndio wanaohusika na upandishaji huo kwa kununua tiketi na kuziuza tena kwa abiria kwa bei kubwa, na wala sio kampuni,” alisema Meneja wa Kampuni ya Mabasi ya Master City Ltd, Miraji Mgongolwa.

Hata hivyo, maelezo ya baadhi ya makarani hao waliokuwa wanadai kutokupanda kwa nauli hizo, kunakinzana na nauli aliyotozwa abiria mmoja aliyekuwa anasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza baada ya kukatiwa tiketi ya Sh. 38,000 tofauti na na ile ya 35,400 iliyotajwa kutozwa na Kampuni ya Master City.

“Naenda Mwanza, nimelipa nauli ya Sh. 38, 000,” alisema Mwita Wilson (25) akiwa UBT muda mfupi baada ya kukata tiketi. Kinyunyu George, Karani wa Kampuni ya Mabasi ya Mapanda, alisema kuwa nauli bado hazijapanda kwani Sumatra wapo wakivinjari kituoni hapo huku wakiwauliza abiria iwapo wametozwa nauli zaidi ya ile iliyopangwa na ma
mlaka
EXPERTS ,from German  have  called upon Tanzanian  government to exercise maximum care in uranium exploration and extraction to ensure the mineral does not affect people’s health.

“There is no way that you can mine uranium without damage to the environment. Experience all over the world shows that there is no way people can mine uranium properly without damaging the environment or endangering the health of the people,” said the chairman of the Germany-based Uranium Network, Gunter Wippel.


He gave the advice at a news conference organised by the Legal and Human Right Centre (LHRC) to share experiences on uranium mining in his home country.


Wippel cited the example of Germany, saying despite having money and technological capacity it is compelled to spend at least 7.0 billion Euros to maintain all mines after uranium extraction.


Thousands of German uranium miners, he said, died of lung cancer for working in poorly vented underground shafts in the 1950s.


He said for Tanzania, like other countries, discharge of radioactive and poisonous contaminants as well as other effects of mining such as heavy freight, traffic, water consumption will challenge the integrity of the mining area.


Wippel said dealing with uranium mining was more hazardous than other types of mining because of its long term effects.


The expert noted that uranium mining hazards are enhanced by local risk factors which include large-scale flooding during the rain season, safety of mine facilities, direct exposure of people to dust and water due to traditional life styles.


“Due to the shallow nature of the uranium deposits at Bahi and Manyoni, it is likely that people get in contact with elevated radiations and wells might be contaminated naturally. However this phenomenon needs to be examined in depth before drawing any conclusion,” he said.


Another expert, Martin Kurz, said his organisation was informed about Bahi district being subjected to uranium exploration by its partners in 2008.


“We were scared about how the people will be affected. I got in touch with Gunter and we’ve informed ourselves on the problem of mining and we are still thinking of how it threatens people’s lives at the area,” he said.


LHCR acting executive director Imelda Urio urged the government to halt its plan of uranium exploration and extraction and look alternative sources of income because of the metal’s adverse effects.

 “We advise the government to find alternative sources of income to rejuvenate the national economy or for increasing revenue instead of dealing with uranium exploration,” she said.
She said research carried out by her organsation has shown that people living in areas surrounding uranium exploration projects were ignorant of the hazardous mineral, nor do they know its uses or advantages.

When contacted for comment on the matter, Deputy Minister for Energy and Minerals Stephen Masele said the government has not issued any permit for uranium extraction pending environmental impact assessment by the National Environmental Management Council.

Monday, December 3, 2012


 Grant to support regional integration initiatives,


The EAC and  have signed a financial grant agreement worth 30 million Norwegian Krone (approximately US $5.3 million) for the period 2012 to 2014.
EAC Secretary General Amb. Dr. Richard Sezibera and Norway’s Ambassador to the United Republic of Tanzania with an accreditation to the Community, Her Excellency Ms. Ingunn Klepsvik, signed on behalf of EAC and Norway respectively.
The funds, disbursed through the EAC’s basket fund mechanism known as the Partnership Fund, will support initiatives to enhance regional integration and socio-economic development of the EAC.
A press release from EAC communication department suggested stated  that  the funds will be used to support the implementation of the EAC Development Strategy and provide technical assistance to the Community.
It further elaborated that the grant will support institutional and human resource capacity building for the EAC and support key studies required to support regional integration as well as implementation of the study findings.
According to the agreement, an initial disbursement of 10 million Norwegian Krone (approximately US $1.8 million) will now be made by Norway’s Ministry of Foreign Affairs.
Norway is one of the founding members and a contributor to the EAC Partnership Fund
Also present at the signing ceremony was the head of the resource mobilization unit at the EAC, Dr. James Njagu

Sunday, December 2, 2012


Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa ( Pichani juu wa pili kushoto) akijumuika pamoja na Baadhi ya Wabunge wanaounda timu ya Bunge Sports inayoundwa na wabunge kutoka Baraza la Wawakilishi na Bunge la Jamhuri,wakati wa Chakula cha Mchana alichowaandalia Nyumbani kwake, Ngarashi Wilayani Monduli mwishoni mwa wiki iliyopita.
Wengine kwenye picha ya kwanza juu kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo,Mh. Amos Makalla, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni,Mh. Iddi Azzan pamoja na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Monduli, Reuben ole Kunai.

Saturday, December 1, 2012

PICHA MBALIMBALI ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI UKIMWI
WAGENI NAO WALIKUWA MAKINI KUFUATILIA MATUKIO YA MAADHIMISHO YA UKIMWI
RAIS KIKWETE AKIWAHUTUBIA WANANCHI





AFRICAN research consortium Biannual Research Workshop which is expected to bring together 200 researchers, academics, policy-makers and other economists who participate in the Research Programme will convene on Sunday in Arusha Tanzania  to discuss Gender Economic development in Africa

 The workshops  which will take place  at Mount Meru Hotel will provide  a forum in which the participants can meet each other within a worldwide network of professionals, and deal with issues relevant to Africa’s economic development.

The session, which will be chaired by Prof. Charles Soludo, former Governor Central Bank of Nigeria and now, the Chairman of Institute for African Heritage, Nigeria will feature four presentations by distinguished economists. Stephanie Seguino of University of Vermont, USA, and Maureen Were, Central Bank of Kenya,  who will start off the proceedings with a look at Gender, Development and Growth in Sub-Saharan Africa.

A press release issued by AERC communication  stated that other papers expected to be presented will be Collecting Gender Disaggregated Data to Improve Development Policies by Cheryl Doss, Yale University, USA and  the the third paper will be Gender and Economic Empowerment in Africa and   Evidence and Policy Issues by Naomi Wekwete, University of Zimbabwe.

The last paper on The Care Economy in Africa Subsistence Production and Unpaid Care will be presented by Nancy Folbre, University of Massachusetts, USA.



MBUNGE VITI MAALUM MAGIGE KATIKA PICHA YA PAMOJA NA BAADHI YA WALEMAVU WALIOPATIWA BAISKELI  MAALUM KUWASAIDIA KUTEMBEA

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews