Wednesday, November 28, 2012

Rais Mursi wa Misri anapingwa kwa kujilimbikizia madaraka

Majaji wa mahaka ya rufaa nchini Misri wanajiandaa kususia kazi na kuunga mkono waandamanaji dhidi ya rais wa misri Mohammed Morsi kujipa mamlaka zaidi.
Sheria ya kumapaka mamlaka zaidi rais Mursi ilipitishwa siku ya Alhamisi wiki jana. Sheria hiyo inampa mamlaka rais kuchukua hatua zozote kulinda mapinduzi na kusema kuwa hakuna mahakama yoyote inaweza kuamua vinginevyo.
Hatua hii ilizua hasira miongoni mwa wananchi kote Misri.
Polisi wamefyatua mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliopiga kambi kwenye medani ya Tahrir kupinga uamuzi wa rais Morsi kujitangazia madaraka makubwa.
Picha za televisheni zimeonyesha waandamanaji walioficha nyuso wakiwarushia polisi mikebe ya mabomu hayo ya kutoa machozi.
Hapo jana waandamanaji hao walifanya maandamano na kuimba nyimbo za kumlaani Rais Morsi pamoja na vuguvugu lake la kiislamu la Muslim Brotherhood.
Walikesha usiku kucha katika medani ya Tahrir mjini Cairo kuelezea hasira zao dhidi ya tangazo la rais wao anayezingatia itikadi za kiislamu Mohammed Morsi kujipatia madaraka makubwa.
Walikesha wakiimba nyimbo za kumlaani rais pamoja na vuguvugu lake la kiislamu la Muslim Brotherhood.
Jana Jumanne, maelfu ya waandamanaji walifurika katika medani hiyo wakiandaa mandamano kadhaa huku wakisema watamkiuka rais Mursi huku wakipinga mamlaka aliyojilimbikizia.
Maandamano mengine ya kumpinga rais Morsi yamefanyika katika maeneo mbali mbali nchini humo.
Bwana Morsi amejaribu kumaliza mzozo huo kwa kuahidi kuwa madaraka yake yatakuwa na kikomo.
Vuguvugu la Muslim Brotherhood, ambalo bwana Mursi ni mwanachama, liliakhirisha mkutano wao siku ya Jumanne likisema linataka kuzuia taharuki kutanda miongoni mwa wanachi.
Waandamanaji wanasema Rais na chama chake cha Muslim Brotherhood wanajipatia mamlaka kinyume na sheria
Lakini lilisema linauwezo wa kukusanya mamilioni ya watu wanomuunga mkono rais wao.
Wanaomuunga mkono bwana Mursi wanasema kuwa sheria hiyo inahitajika ili kulinda mafanakio yaliyotokana na mapinduzi ya kiraia dhidi ya utawala wa Mubaraka na idara ya mahakama ambayo ilikuwa na watu wanaomuunga mkono rais aliyng'olewa mamlakani.
Waandamanaji wanasema kuwa vuguvugu la Muslim Brotherhood limeyateka nyara faida zilizotokana na mapinduzi ya kiraia. Source :BBC Swahili

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Blog Archive

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews