Thursday, November 29, 2012



MBUNGE wa Jimbo la Arumeru Mashariki  kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Joshua Nasari  amesusia kikao cha Baraza la Madiwani  wa  Halmashauri ya Meru ,baada ya kamati ya Uchumi ,Ujenzi  na Mazingira ,kutaka kupitisha azimio la kugawa viwanja eneo la Soko la Tengeru.
Mbunge huyo alidai kuwa alichukua uamuzi  huo baada ya kuona baraza hilo kukiuka makubaliano ya awali ya kujenga vitega uchumi katika eneo hilo na kudai kuwa anahisi kuna mchezo  wa kifisadi unaotaka kufanywa.
“Awali tulikubvaliana kujenga vitega uchumi leo wabadilisha kinyemela wanataka kutengeneza mlango wa kufanya ufisadi siwezi kushiriki kubariki jambo hilo kamwe”alisema Nassari akizungumza na waandishi wa habari. 
Alisema kuwa ana historia  ndefu iayoonyesha kuwa siku zote  Viwanja vikitolewa wanaokuja kununua ni watu wa Arusha mjini ,watu wa Moshi na watu wa Meru hawaambulii chochote.
Alisema kuwa  kwa maoni yake ni faida zaidi kujenga vitega uchumi  ili wananchi waje wafanyie biashara badala ya kugawa kama Kamati ya Uchumi ilivyopendekeza. 
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Frida Kaaya akielezea sakata hilo aliliambia Baraza hilo kuwa ameshangazwa na maamuzi ya Mbunge huyo ambaye alisema ni Diwani akiwa katika Baraza hilona alipaswa  kukubali maamuzi ya Madiwani wenzake .
Alisema kuwa viwanja vinavyotarajiwa kugawanywa ni Viwanja 118 ,vitakavyojengwa kuzunguka soko na hivyo kufanikiwa kuwaondoa wafanyabiashara wanaopanga bidhaa chini .
Alifafanua kuwa kwa sasa Halmashauri hiyo imeanza kujikita kusaidia Vijana ,na kuwa kugawanywa viwanja hivyo kutalenga vikundi vya vijana ,ili waweze kufungua miradi ya maendeleo  kupitia vikundi,hatimaye kuweza kujikwamua katika uchumi na kuongeza kipato chao .
Diwani wa Kata ya Nkwarusambo akizungumza katika kikao hicho alimtaka Diwani Nassari kuheshimu maamuzi ya vikao  vya baraza na kushirikiana na madiwani wenzake kulewatea wananchi maendeleo na siyo kupinga kila kitu hata kama ni jambo jema .
Alisema kuwa Halmashauri hiyo ,inasifiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wananchi ,na kuwa Mbunge huyo anatakiwa kuepuka migogoro isiyokuwa na na lazima .


0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Blog Archive

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews