Sunday, December 15, 2013


WATU sita wamefariki dunia popo hapo katika ajali mbaya iliyotokea katika barabara ya Arusha Namanga eneo la Longido Mkoani Arusha likihusisha gari dogo la abiria na lori la mizigo.
Gari la abiria  lililoua watu sita  




Tukio hilo ambalo limethibitishwa na Jeshi la polisi Mkoani Arusha lilitokea  5 za usiku wa kuamkia jana na kusabaisha abiria sita waliokuwa katika gari dogo aina ya noa kupoteza maisha baada ya gari dogo aina ya Noah kugongana uso kwa uso la lori la mizigo.

Mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa gari dogo ambalo lilikuwa likitokea Arusha likiwabeba wapishi waliokuwa wakitokea jijini Arusha kwenda Longido kwa ajili ya sherehe za kipaimara na harambee  ya kumalizia ujenzi wa kanisa la KKKT.

Harambee hiyo ilikuwa iongozwe na waziri Mkuu mstaafu Edward Lowasa na katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana.

“Nilikuwa wa kwanza kufika katika eneo la ajali nilishiriki kutoa miili sita ya watu waliopotea maisha wengine wawili walikuwa na hali mbaya wapo Hospitali “alisema Sendeu Parmwat shuhuda na mkazI wa Longido.

Parmwat alisema kuwa watu wote waliofariki papo ni wapishi waliokuwa wakiongozwa na mtaalamu wa mapishi anayejulikana kwa jina maarufu la Bonge Jijini hapa.
Alisema kuwa polisi walifika muda mfupi na kuanza kuchukua miili ya marehemu pamoja na kuwapeleka majeruhi katika hospitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru.
Shuhuda mwingine Stephano Laiser alieleza kuwa lori lililosababaisha maafa hayo lilikuwa limepaki pembeni ya barabara na halikuwa na taa.
Akizungumzia kuhusu ajali hiyo kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Arusha Liberartus Sabas alisema kuwwatu hao wali[poteza maisha na wengine wawili wamelazwa hospitali ya Mkoa wa Arusha ya  Mount Meru.
“Abiria sita katika Noa yenye namba T 329AWJ  walipoteza maisha na hakuna majeruhi yeyote katika lori ,tunaendelea na uchunguzi lakini taarifa za awali zinaonyesha kuwa Noa ilikuwa katika mwendo kasi”alisema Kamanda Sabas.  
Aliwataja marehemu waliotambuliwa  kuwa ni Hamidu Msala maarufu kwa jina la Bonge,Habibu waziri ,Faridah Ibrahim ,Martha Gabriel wote wakazi wa Jiji la Arusha wengine wawili bado hawajatambuliwa.
Waandishi wa habari walishuhudia  ndugu jamaa za marehemu wakiwa katika uwanja wa eneo la kuhifadhi maiti katika hospitali ya Mkoa wa Arusha kufuatilia habari za ndugu zao.
Naye muuguzi wa zamu katika hospitali ya Mount Meru ambaye hawakuwa tayari kutaja jina alithibitisha kuwepo kwa majeruhi  wawili ambao alisema hali zao ni mbaya.
“Wako katika uangalizi wa juu ,majreha ni makubwa sana mmoja yuko hoi lakini tunajitahidi kuokoa maisha yao”alisema Muuguzi huyo.
Mwisho……



0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews