Saturday, March 9, 2013


Uhuru Kenyata  aameshinda  kiti cha urais kupitia Muungano wa Jubelee  katika uchaguzi ulio malizika  kwa kura kuhesabiwa na kuhakikiwa katika makao makuu ya ya kuhesabu kura  katika eneo la Bomas  Jijini a Nairobi.
Kufikia  saa  8:30 usiku  Uhuru alikuwa mbele kwa kura 6,173,433 dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga aliyekuwa na kura 5, 340,546 ikiwa ni tofauti ya kura 832,887 na majimbo yaliyo kwisha kutangazwa ni 291/291.


Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC jumla ya kura zote zilizopigwa na kuhesabiwa  kwa nafasi ya Urais ni kura 12,338, 667 kutoka katika majimbo yote ya Uchaguzi 291 huku kura zilizoharibika zikiwa 108975 na kura halali zikibaki 12,222,980.

Katika kinyang’anyiro hicho Wycliffe Musalia Mudavadi anashika nafasi ya tatu akiwa amejikusanyia kura  483,981 nafasi ya nne ikienda kwa Peter Kenneth mwenye kura 72,786.

Mgombea wa Alliance for Real Change,Mohamud Abduba Dida anashika nafasi ya tano akiwa na kura  52,848 akifuatiwa na Mwana mama Martha Karua wa National Rainbow Coalition mwenye kura 43,881 hadi sasa.

Nafasi ya saba katika wagombea hao Urais inakwenda kwa James ole Kiyiapi wa Chama cha Restore and Build Kenya ambaye ana kura 40,998 huku nafasi ya ya nane na mwisho ikishikwa na Paul Kibugi Muite wa chama cha Safina.
Matokeo hayo yatatangazwa rasmi leo saa saa 5  asubuhi,


0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews