Friday, January 3, 2014


WATU wawili wamefariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi katika machimbo ya kokoto katika eneo la Terat nje kidogo ya Jiji la Arusha.
Kufuatia tukio hilo  serikali mkoani Arusha imepiga marufuku uchimbaji wa kokoto katika eneo hilo na kuagiza kamati iliyoundwa mwaka jana baada ya ajali kama hiyo kutokea katika eneo la Moshono  kufanya uchunguzi katika migodi yote.

Kwa mujibu wa Mulongo kamati hiyo itatakiwa kuleta mapendekezo  na kuleta mapendekezo ya namna ya  kuboresha hali ya usalama katika machimbo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa  Mulongo ametoa amri hiyo baada ya kufika katika eneo la tukio na kuongea na viongozi wa eneo hilo.

“Ile kamati sasa itaanza upya kuchunguza hali ya usalama na kuleta mapendekezo  ya kuhakiki hali ya usalama”alisema Mulongo.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Arusha Liberatus Sabas aliwataja waliopoteza maisha kuwa ni Joseph Solomon  (18)na Saimon Petro(15) wote wakazi wa Muriet.

 Katika hatua nyingine jeshi   la polisi Mkoani  Arusha kupitia kwa kamanda Liberatus Sabas limewataka watu wanaomiliki migodi ya uchumbaji wa kokoto kuhakikisha kuwa wana vibali vya kufanya kazi hiyo.

“Tunapiga marufuku haya machimbo yanayoanzishwa kiholela na kuhatarisha maisha ya watu ,tutaanza kufuatilia na kuchukua hatua kwa kushirikiana na vyombo vingine vya serikali”alisema Sabas.
Aliongeza kuwa pia katika migogodi hiyo wahakikishe kuwa kuna usalama wa kutosha ikiwemo miundo mbinu ya tahadhari  na uokoaji.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa lilitokea saa tatu asubuhi leo katika machimbo hayo baada  ngema kuwaangukia vijana waliokuwa wakichimba na kupakia moram katika gari lililofika katika machimbo hayo.
“lilitokea ghafla sana mimi nilikuwa juu mara nikasiakia ngema inakatika yaani nilishuhudia wenzangu wakifunikwa na udongo na kupoteza maisha”alisema manusura Loiruk Sandamu.
Tukio hilo ni la pili kutokea katika machimbo ya kokoto Jijijni Arusha baada ya mwaka  Machi 16 mwaka jana  kuanguka na kufukia watu 16 katika eneo la Moshono.


0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews