Tuesday, May 7, 2013


WAFUGAJI wa kabila la Kimaasai wametakiwa kuuza mifugo na kusomesha watoto wao ili wapate elimu itakayowawezesha kupata fursa mbalimbali za kiuchumi ,kijamii na kisiasa  kama jamii zingine hapa nchini.
Wito huo ulitolewa na Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari katika harambee ya ujenzi wa shule ya Sekondari katika eneo la Ngabobo Wilayani Arumeru.
Nassari alisema kuwa jamii hiyo ipo nyuma katika Nyanja za  kimaendeleo  kutokana na kuendelea na mfumo wa ufugaji wa kuhamahama jambo ambalo limesababaisha watoto wengi  katika jamii hiyo kukosa fursa ya kupata elimu.
“Nawasihi  ndugu zangu wamasai sasa muanze kuwekeza katika elimu kwa watoto wenu ,nyakati hizi hakuna njia nyingine ya kutatua changamoto ni elimu pekee ndio njia ya kuweza kuleta faida isiyokwisha katika maisha yenu”alisema Nassari.
Aidha Mbunge huyo aliwapongeza wananchi wa eneo hilo kwa kujitokeza kwa wingi na kutoa mifugo kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo na kusema kuwa huo ndio mwanzo mpaya wa jamii hiyo kuanza kubaduilika kwa dhati na kuthamini elimu.
Aliwaambia wafugaji hao kwamba jamii hiyo imekuwa ikitoa viongozi waadilifu na wachapa kazi akiwemo waziri Mkuu mstaafu Edward Moringe Sokoine na Edward Lowasa.
“Kwa asili mmejaliwa kuwa na watu wenye mismamo na maamuzi yenye masilahi kwa umma ,wasomesheni watoto wenu ili waweze kutoa mchango katika kujenga taifa letu katika nynaja za kiuchumi na hata kisiasa”alisema Nassari.
Aliwaambia wafugaji hao kuwa yeye alisoma katika hali ngumu na wakati fulani akisoma shule ya sekondari wazazi wake walilazimika kuuza kabati la vyombo ili apate ada.
Alisema aliweza kusoma vizuri na kumaliza chuo kikuu ambapo sasa ana uwezo wa kununua kila nachokihitaji katika maisha yake na jamii yake.
Katika harambee hiyo wananchi walitoq ngombe zaidi ya 50 zenye thamani ya shilingi milioni 15 mbuzi na kondoo wenye tahamni ya shilingi milioni 7
Katika harambee iliyoendeshwa na mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha Onesmo Nangole  kwa niaba ya  Waziri   Mkuu mstaafu Edward Lowasa jumla ya shilingi milioni 53 zilipatikana

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews