Sunday, June 16, 2013




WATU wawili  wameripotiwa kupoteza maisha na
wengine zaidi ya hamsini kujeruhiwa  katika tukio la mlipuko wa kitu kinachodhaniwa kuwa bomu la kutengenezwa kwa mkono katika mkutano  wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa kata nne za jiji la Arusha  unaofanyika leo.
Tukio hilo limetokea  majira ya saa 12 kasoro katika kata ya  kaloleni kwenye uwanja wa michezo wa Soweto Jijini hapa
Hata hivyo taarifa za hivyo hivyo havijathibitishwa na vyombo vya usalama Mkoani Arusha hadi kufiklia alfajiri ya leo na kutokana na hali ya tharuki iliyokumba Jijij la Arusha jana jioni baada ya tukio hilo kutokea katika mkutano huo am,bao ulihutubiwa na mwenyekiti  wa Chadema Taifa  Freeman Mbowe.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo inaelezwa kuwa mlipuko ulitokea karibu na gari la matangazo wakati makada wa cha,ma hicho wakikusanya sadaka zilizodaiwa kuwa zingesaidia mawakala wa chama hicho katika zoezi la kulinda masilahi ya chama hicho katika uchaguzi huo.
Waandishi wa habari walishuhudia idadi kubwa ya majeruhi wakitibiwa katika hospitali za Seliani na Mount Meru wengi wakiwa na majeraha miguuni ,usoni na mikononi.
Kamanda wa Jeshi la polisi           Mkoani Arusha Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kukataa kusema lolote na kuahidi kutoa taarifa kamili za tukio hilo leo mchana.
Tukio hili ni la pili kutokea katika kipindi kisichozidi miezi miwili baada ya shambulizi la aina hiyo kufanyika katika kanisa la Katoliki parokia Olasiti nje kidogo ya Jijiji la Arusha na kusababisha vifo kadhaa namajeruhi.

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews