Monday, May 6, 2013


IDADI, ya watu waliopoteza maisha katika shambulio la wa bomu ililolipuka katika sherhe za uzinduzi wa kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yosef Olasiti imeongezeka na kufikia wawili.

Majeruhi aliyefariki jana usiku ametambuliwa kuwa ni James Gabriel (16) 

Hali kadhalika majeruhi wwengine hali zao ni mbaya na wapo katika chumba cha uangalizi maalum katika hospitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru.

Hadi asubuhi ya leo hakuna majeruhi walioruhusiwa kurudi nyumbani  na majeruhi mmoja alikimbizwa jana katika hospitali ya rufaa ya KCMC  Mkoani Kilimajaro.

Wakati huo huo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Gharib Bilal na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini  Inspekata Jenerali  Said Mwema wamewaasili Jijijni Arusha na kuwatembelea majeruhi wa bomu ililolipuka katika sherhe za uzinduzi wa kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yosef Olasiti.

 lililolipuliwa kati kati ya waumini wa wa kanisa Katoliki la Parokia ya Mtakatifu Joseph na kusababaisha kifo cha mtu mmoja na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa vibaya.

Dr.Bilal aliwasili katika hospitali ya Mkoa wa  wa Arusha Mount Meru akiongozana na Mkuu wa kanisa la kiiinjili la Kilutheri Dr,Alex Malausa pamoja na viongozi wa madhehebu kadhaa ya dini Mkoani Arusha.

Akizungumza na majeruhi hao Makamu wa Rais aliwahakikishia majeruhi hao kuwa serikali itatumia nguvu  zote  za ulinzi na usalama kuwatia mbaroni watuhumiwa wa tukio hilo.

Wakati huo huo watu sita wanashikiliwa na polisi kufuatia tukio hilo ambalo kwa mara ya kwanzalinatarajiwa kuongeza hofu na mashaka juu ya usalama kwa wananchi  hasa katika mikusanyiko na sehemu za kupata huduma mbalimbali za kijamii.

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews