Wednesday, August 7, 2013



Hospitali ya Misheni ya Kolandoto katika Wilaya Shinyanga mjini  inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuwahudumia watu waisho  na virusi vya ukimwi kufuatia kukosekana kwa mashine ya kuhesabu kinga za mwili (CD4) katika hospitali hiyo.

Mashine hiyo inaelezwa na wataalamu  wa tiba kujua kinga za mwili za mwathirika wa virusi vya ukimwi ili kujua iwapo anastahili kuanzishiwa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi ARV.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo juzi, Kaimu Mganga Mkuu  Dr.Phares Bwire alieleza kuwa ukosefu  wa mashine hiyo umekuwa ukisababaisha kuharibika kwa sampuli za damu ambazo zinalazimika kuplekwa  hospitali ya Mkoa wa Shinyanga kwa vipimo zaidi.

Alisema hospitali hiyo ilipata msaada wa mashine mbili za kupima damu (Screen Master na Full Blood Picture) kutoka Shirika la Afya linalojishughulisha na vita dhidi ya Ukimwi na Utoaji wa Huduma za Kujikinga, Matunzo na Tiba kwa wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi (AGPAHI).

“Tunakabiliwa na changamoto katika utoaji wa huduma kwa  Waviu naomba wadau wengine wajitokeze kutusaidia kama walivyofanya  shirika la afya linalojishughilisha na mapambano ya ukimwi ,tiba na matunzo kwa  wagonjwa wa ukimwi AGPAHI… ukosefu wa mashine hii muhimu  ya kuhesabu CD4 unasababisha kuharibika kwa baadhi ya sampuli za damu.

Alisema kuwa wakati mwingine majibu ya CD4  yanachelewa kufika ambapo wanalazimika kusubiri kwa siku zisizopungua 14 hadi mwezi mmoja jambo linalowafanya wagonjwa kukata tamaa na wengine kukimbia matibabu

Kwa mujibu wa mganga huyo huduma za kupima na kutoa  dawa za ARV kwa   waathirika wa VVU zilianzishwa hospitalini hapo mwaka 2007  kwa ushirikiano na shirika la AGPAHI.

Mganga huyo alisema mbali na msaada wa mashine hizo, AGPAHI imewezesha mafunzo kwa watoa huduma wa kliniki za waathirika wa VVU, watoa hduma majumbani, vitendanishi, ukarabati wa majengo na dawa za ARV.

“Tangu tumeanza na shirika hili mpaka sasa ni zaidi ya sh milioni 200 za AGPAHI zimetumika kwenye shughuli mbalimbali hospitalini hapa hivyo tunaomba na mashirika mengine wajitokeze kutusaidia maana wagonjwa ni wengi,” alisema Dk. Phares.

Awali alibainisha kwamba hadi sasa waathirika zaidi ya 831 wanahudumiwa hospitalini hapo kwa dawa na ushauri huku akibainisha kwamba kati ya waathirika hao 70 ni watoto chini ya miaka 14 ambapo waathirika 114 wanatumia dawa za ARV wakati watoto wanaopewa dawa hizo ni 39.

Mwisho…

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews