Friday, February 8, 2013


FAMILIA ya marehemu  Baba skofu Thomas Laizer wa Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania dayosisi ya kaskazini kati imesema kuwa hayati Baba askofu ameacha wosia mzito kwa waumini, wachungaji na viongozi wa kanisa hilo baada ya yeye kupita.
Akizungumza nyumbani kwa askofu huyo katika eneo la Nduruma mke wa askofu huyo Mama Maria Laizer alisema kuwa mume wake kila mara alikuwa anasisitiza kuwa kazi aliyoianzisha iendelezwe na isiharibiwe kwa vyovyote vile.
“Baba  askofu alisisitiza jambo hili hata kwa wote waliofika kumjulia hali akiwa kitandani kwake kuwa wahakikishe kuwa kazi aliyoianza inaendelezwa “alisema Mama Laizer.
Alileza kuwa alikuwa na mume wake masaa machache kabla ya kifo chake na kwamba mchana wa siku aliyoaga dunia alikuwa na hali nzuri lakini baadye hali yake ilibadilika na kuondokewa na uhai.
Alisema kuwa askofyu huyo alianza kusumbuliwa na maradhi ya kansa kwa kipindi cha miaka minne iliyopita lakini hakuweza kupata tiba stahili kwa haraka.
“Alikuwa akilalamika maumivu katika tumbo lake mara kwa mara na baadaye alizidiwa tukampeleka Nairobi akatibiwa lakini baada ya muda alianza tena kulalamika maumvu na ndipo akapelekwa India na kugundulika kuugua kansa ambayo tayari ilikuwa imesambaa mwilini”alisema Mama Laizer.
Marehemu Baba askofu Thomas Laizer ameacha mjane watoto wanne na mjukuu mmoja.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews