Friday, February 1, 2013


__
Mkurugenzi wa TACTO Freddy Massawe akijibu maswali yaa waandishi wa habari hawaonekani katika picha
Mkurugenzi mtendaji wa chama cha wafanyabiashara wa utalii wa kitamaduni nchini(TACTO) Fred Massaweakionyesha moja ya picha za wachoraji kutoka Tanzania zitakazoonyeshwa katika tamasha kigali
Tanzania inaandaa msafara wa watu mia na ishirini kwenda kuiwakilisha katika tamasha la sanaa na utamaduni la jumuiya ya Afrika Mashariki  litakalofanyika Kigali nchini Rwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi mtendaji wa chama cha wafanyabiashara wa utalii wa kitamaduni nchini(TACTO) Fred Massawe alisema kuwa tamasha hilo litafanyika mwezi huu.

Ameeleza kuwa tamasha hilo linalenga kuunganisha wananchi wa jumuiya ya afrika mashariki na litakuwa linafanyika kwa mzunguko katika nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.
Alisema kuwa washiriki wa tamasha hilo watakuwa ni wachoraji wachonga vinyago ,ngoma za kitamaduni na washonaji wa shanga na bidhaa mbalimbali zenye sura za kitamaduni.

Akilezea zaidi alisema kuwa utalii wa kitamaduni unaweza una uwezo mkubwa wa kjuinua uchumi wa  hata mtu mmoja mmoja.
Alisema kuwa utalii wa kitamaduni unakadiriwa kuongeza ajira zaidi ya laki moja na kama juhudi za kuutangaza zikifanyika ajira hizo zinaweza kuongezeka maradufu.
Alitoa wito kwa wadau wa utalii na serikali  na wadau wengine kusaidia kuwezesha kupeleka watu wengi zaidi katika tamasha hilo kutokana na nchi kujaa utajiri wa tamaduni zenye  kuvutia.
Alisema kuwa Tanzania ina umuhimu mkubwa wa kushiriki tamasha hilo kutokana na kuwa tamaduni nyingi na vivutio vingi vya asili ambavyo vitaitangaza nchi katika masoko ya utalii.
Mwisho……………….

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews