Thursday, April 25, 2013


Jeshi la polisi linamsaka Mbunge wa Jimbo la Arusha Godbless Lema kwa tuhuma za kuhusika katika vurugu zilizotokea juzi katika chuo cha Uhasibu Mkoani Arusha  na kusababisha chuo hicho kufungwa kwa muda usiojulikana.
Kaimu kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Arusha Kamishna msaidizi wa Jeshi la polisi Ibrahim Kilongo aliwaaambia waandishi habari kuwa jeshi hilo limetoa ilani kwa mbunge huyo kujisalimisha polisi haraka.

“Tunamtaka popote alipo afike mwenyewe  poilisi na bado tunaendelea kumtafuta popote  alipo ,ni muhimu afike tufanye naye mahojiano kuhusu yaliyotokea katika chuo cha uhasibu ”alisema Kilongo.

Kaimu kamnda huyo alikataa kutaja majina ya wanafunzi kadhaa waliokuwa wamekamatwa katika vurugu hizo.

“Tutawapa hayo majina ya wanafunzi tuliwakamata katika tukio hilo  baadaye  kwa sasa tunaendelea kuwahoji ili kupata taarifa muhimu za vurugu zilizotokea  “alisema Kamanda huyo kwa kifupi.

Inadaiwa  kuwa Lema anatuhumiwa kuhusika katika vurugu zilizopekea kudhalilishwa na kuzomewa kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo.

Mara baada ya kutulizwa kwa vurugu hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mgesa Mulongo aliliagiza jeshi l polisi kumkamata Mbunge huyo  kwa kile kilicholezwa kuwa ni kumhusiha na vurugu zilizotkea chuoni hapo.

Hata hivyo Mbunge huyo alikana vikali kuhusika katika vurugu zozote na kueleza kuwa alitumia nafasi yake kuwashawishi wananfunzi kurudi chuoni na kisha akawasiliana na Mkuu wa Mkoa kufika kuzungumza na wanafunzi hao.

Katika tukio hilo  lililosababisha mabomu ya machozi kurindima kwa kwa muda katika viunga vya chuo hicho Mkuu huyo wa Mkoa alijikuta akizomewa baada ya kushindwa kuhutubia mamia ya wanafunzi baada ya kukosekana kwa kipaza sauti.

Awali wanafunzi hao walitaka kuandamana kuelekea kituo  kikuu cha polisi Jijini hapa kufuatia mwanafunzi mwenzao kuuawa katika mazingira waliyodai yana utata karibu na chuo hicho usiku wa kuamkia siku ya  jumatano wiki hii.

Baadhi ya wananchi waliohojiwa na gazeti hilo kutoka maeneo ya Njiro Peter Muinisi na Fredy Swat walisema kuwa wameshangazwa na hatua ya Mkuu wa Mkoa kumnyooshea Lema kidole na kuagiza akamatwe kuhusiana na tukio hilo.

“Hii ni aibu tulimwona Lema akiwabembeleza wanafunzi wasiandamane  kwenda kati kati ya mji  ,alitaka jambo hilo litafutiwe ufumbuzi bila kuleta madhara yoyote,hebu fikiri wanafunzi wale wangefika kati kati ya mji hali ingekuwaje”alihoji Muinisi.

Aidha alisema viongozi wanapaswa kuheshimiana na kutenda kazi bila kuweka sababu za kibinafsi katika mambo ambayo majibu yake yako wazi mbele ya umma na kutengeneza picha mbaya kwa viongozi.

0 comments:

Post a Comment

Time Management

Translator

Popular Posts

Fellow Bloggers

Popular Posts

Visitors Worldwide

Total Pageviews